Baadhi ya mabomba yatakayotumika kwenye mradi wa Bomba la Mafuta la Afrika Mashariki (EACOP).
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.Dkt. Doto Biteko (katikati), Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba (Wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Nishati, Ziana Mlawa (wa tatu kutoka kulia) wakiimba wimbo wa Wafanyakazi wa Mshikamano wakati Mhe. Dkt. Doto Biteko alipofungua Mkutano wa Tano wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Nishati tarehe 18 Machi 2024 jijini Mwanza.
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakiongozwa na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga wakikagua mradi wa ujenzi wa njia kuu ya umeme wenye msongo wa kilovoti 400 katika eneo la Lemugur Mkoani Arusha, tarehe 13 Machi, 2024.
Muonekano wa jengo la Wizara ya Nishati baada ya kukamilika kwake katika Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio (kulia) akipokea maua mara baada ya kuwasili rasmi katika Ofisi za Wizara ya Nishati, Mji wa Serikali-Mtumba jijini Dodoma tarehe 11 Machi, 2024.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko (wa Nne kutoka kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri na viongozi waandamizi kutoka Wizara zinazohusika na Sekta ya Nishati mara baada ya kikao chao katika Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri wanaohusika na mfumo wa pamoja wa umeme kwa nchi za Mashariki ya Afrika (EAPP Council of Ministers) ambao unafanyika kwa siku mbili jijini Nairobi nchi Kenya.
Muonekano wa mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) wa megawati 2,115
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko (wa nne kushoto) akikata utepe kuashiria uwashaji umeme katika Kijiji cha Ikwavila wilayani Wanging’ombe mkoani Njombe. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Antony Mtaka na wa tatu kutoka kulia Mbunge wa Wanging’ombe Dkt.Festo Dugange.
Mitambo ya kuchoronga visima vya uhakiki (drilling rig) kwa miradi ya Jotoardhi nchini ikiwa imefungwa katika chanzo cha Jotoardhi cha Ngozi (70MW) wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko, akisalimiana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mbeya, mara baada ya kuwasili kwa ziara ya kikazi mkoani humo.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akishuhudia utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mradi wa uzalishaji umeme wa megawati 49.5 kwa nguvu ya maji katika Mto Malagarasi mkoani Kigoma. Wanaosaini ni Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga (kulia) na Meneja Mradi kutoka kampuni ya Dongfang Electric International ya nchini China, Ni Zhihong. Hafla ya utiaji saini imefanyika jijini Dodoma, tarehe 08 Februari, 2024.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na watendaji mbalimbali wa Serikali na kampuni ya EACOP kabla kukagua kazi mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya kuhifadhi mafuta ghafi kutoka Uganda katika kata ya Chongoleani jijini Tanga. Katika ziara hiyo aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Waziri Kindamba na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na ujumbe kutoka Misri ukiongozwa na Waziri wa Nyumba, Nishati na Maendeleo ya Makazi wa nchi hiyo, Mhe. Assem Elgazzar katika kikao kilicholenga maendeleo ya mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) kilichofanyika jijini leo Disemba 21, 2023 Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga (katikati) akitembelea na kukagua Miundombinu ya Upakuaji wa Mafuta ya aina yote yanayoingia
na kutoka nchini wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wakala huo, Tarehe 09 Januari, 2024 Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko
akitambulisha viongozi mbalimbali waliofika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam kwa ajili ya
kumpokea Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Liu
Guozhong ambaye amewasili nchini kwa ziara ya siku Tatu.
Nguzo zikiwa zimepangwa na nyingine kutandazwa chini zikisubiri kukauka kwa kutumia miale ya jua katika moja ya viwanda vya nguzo mkoani Iringa.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akiangalia sehemu ya ujenzi wa mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ambapo alizindua tukio la uchepushaji wa maji ya mto Rufiji kwenye handaki ili kupisha ujenzi wa tuta kuu la bwawa la kufua umeme mkoani Pwani, Novemba 18, 2020.