DKT. BITEKO AZIPONGEZA SSF NA TOTAL ENERGIES KUFIKIA VIWANGO VYA JUU VYA USALAMA VYA USAFIRISHAJI
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezipongeza Kampuni za Total Ernergies na Super Star Fowarders – SSFkwa kuweza kufikia viwango vya juu vya usalama vya usafirishaji huku akiwataka wasafirishaji wengine kufuatanyayo zao kwa kuwa kampuni hizo ni mfano mzuri wa kuigwa.
Dkt. Biteko amesema hayo Juni 25, 2025 jijini Dar es salaam wakati akishiriki katika maadhimisho ya miaka 30 ya ushirikiano kati ya Kampuni ya Super Star Fowarders (SSF) na Total Energies.
“ Leo tumekusanyika hapa kusherehekea hafla ya miaka 30 ya ushirikiano baina ya Kampuni zetu hizi mbili za Total Ernergies na Super Star Fowarders. Katika kipindi hicho chote, mmekuwa washirika wakubwa wa kimataifa katika usafirishaji wa bidhaa mbalimbali hususan kwa kutumia matenki maalum, hakika, binafsi nimefarijika sanana hongereni sana” amesema Dkt. Biteko.
Amesema kupitia ushirikiano huo umewezeshaupatikanaji wa uhakika wa mafuta nchini na kutoa ajira kwa mamia ya vijana pamoja nakuvutia nchi za jirani kutumia Bandari ya Dar Es Salaam kupitishia mizigo yao na kutoa fursa kwa Watanzania.
Ametoa wito kwa wasafirishaji wote wa mizigo kwa kutumia malori nchini wazingatie viwangovya juu vyausalama barabarani kwa kuhakikisha malori yaoyanawekwa vifaa vyote vya usalama kama vile GPS kufuata miongozoi liyopo.
Fauka ya hayo, Dkt. Biteko amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na wafanyabiashara wote na kuwatengenezea mazingira mazuri ya kazi ikiwa ni pamoja na kuweka sera zenye kutabirika ambazo zitawalinda na kuvutia wawekezaji zaidi nchini.
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amewataka wasafirishaji kuzingatia usalama barabarani kwa kuwa suala hilo sio sera tu bali ni kwa maslahi mapana ya Taifa naajali za barabarani zinasababisha hasara kubwa ikiwemo uhai wa watu na uchumi wa nchi. Aidha, ametoa wito kwa wasafirishaji nchini kutumia barabara zilizopo kwa kuzingatia viwango.
Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Anne Sophie amesema siku hiyo ni muhimu kwa Tanzania na Ufaransa kwa kuadhimisha miaka 30yaushirikiano kati ya kampuni hizo mbili ambao umekuwa na faida akitolea mfano mafunzo kwa madereva na matumizi yavifaa na mifumo ya kuzingatia usalama barabarani.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji waKampuni ya Super Star Fowarders (SFF), Bw. SeifA. Seif amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake na jitihada zinazosaidia kuimarisha na kukuza sekta ya usafirishaji nchini.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais Mwandamizi waKampuni ya Total Energies Kanda ya Afrika – Huduma za Masoko, Bw. Jean Phillipe Torres ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na dhamira yake katika kuimarisha sekta ya nishati nchini.