Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko
(katikati) akizindua Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati ya
Kupikia jijini Dodoma tarehe 2 Juni 2025. Kulia kwake ni Naibu Waziri
wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, kushoto ni Lamine Diallo ambaye ni
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu kutoka Umoja wa Ulaya (EU).
Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga akishiriki mjadala kuhusu utekelezaji wa Mpango Mahsusi wa Nishati wa Misheni 300 katika Wiki ya Nishati Jadidifu jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Nishati Mh.Judith Kapinga akizindua kituo Mama cha gesi asilia iliyoshindiwa (CNG) ambacho kina uwezo wa kujaza Gesi Asilia kwenye magari 1200 kwa siku,Mei 9, 2025.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko(wa nne toka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mawaziri wa Nishati wa nchi wanachama wa Umoja wa Soko la pamoja la Kuuziana Umeme katika ukanda wa Mashariki mwa Afrika (EAPP) mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa 20 wa Baraza la Mawaziri wa Nishati wa nchi Wanachama wa Umoja wa Soko la Pamoja la Kuuziana Umeme katika Ukanda wa Mashariki mwa Afrika (EAPP), mkutano huo umefanyika 17 Aprili 2025 Jijini Kampala, Nchini Uganda