11 EAST AFRICAN PETROLEUM CONFERENCE AND EXHIBITION 13
View
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius J. Ndejembi (Mb.), (katikati) akishuhudia utiaji saini wa mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 100, utakaotekelezwa katika eneo la Ngunga, Wilaya ya Kishapu, Mkoa wa Shinyanga.
View
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akipika kwa Nishati safi ya Kupikia (Kuni Poa) alipomtembelea Bi. Afua Juma maarufu kama Mama Manyema, kukambidhi mfumo wa Nishati safi ya kupikia katika eneo lake la kazi Mabibo Jijini Dar es Salaam.
View
Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi kwenye zoezi la uwekaji jiwe la msingi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Ujenzi wa Njia Maalum ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 33 kutoka Kituo cha Kubadilisha njia za umeme (Switching station) cha Masasi hadi Wilaya ya Newala, Mkoa wa Mtwara.
View
Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Nishati, Petro Lyatuu (katikati, waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Nishati waliohudhuria Kongamano la Siku ya Nishati lililofanyika jijini Dar es Salaam sambamba na Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SabaSaba). Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), Mhandisi Charles Sangweni na kulia kwake ni Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Nishati Jadidifu, Mhandisi Imani Mruma.
View
The Crude Oil will be exported via a 2 km long jetty where Tankers can safely be moored and access with sufficient water depth.
View
The Marine Tanks Terminal (MTT) is an Above Ground Installation (AGI). The crude oil, transported by the pipeline will be stored in the Terminal, located on Chongoleani Peninsula in Tanga bay, in 4 tanks of 500,000 barrel each.
View
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tanga ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi. Dkt. Batilda Burian mara baada ya kutembelea mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ambalo utekelezaji wake umefikia asilimia 86.
View
Wataalam kutoka Idara na Vitengo mbalimbali ndani ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake wapo tayari kuwahudumia Wananchi wanaotembelea banda lake katika maonesho ya 50 ya kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
View
Kituo cha kuchajisha vyombo vya moto vya umeme kilichopo Jamatini, jijini Dodoma chenye uwezo wa Kilowati 22 na kina uwezo wa kuchajisha vyombo vitatu vya moto kwa wakati mmoja.
View
Waziri wa Nishati Mhe, Deogratius Ndejembi akiwa katika picha ya pamoja wakati akizindua mradi wa uchimbaji wa visima vitatu ambapo viwili ni kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay na kimoja kwa ajili ya utafutaji huku utekelezaji umefikia asilimia 58 tarehe 27 Februari 2026 mkoani Mtwara
View
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amezindua mradi wa kusambaza mifumo ya umeme jua visiwani unaolenga kuweka mifumo 20,000 ya umeme jua katika visiwa 120 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 8 ambapo Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan ameweka ruzuku hadi ya asilimia 75 katika gharama za uunganishaji umeme.
View
Mradi wa umeme jua wa Kishapu mkoani Shinyanga utakaozalisha megawati 150. Kwa sasa mradi umeanza kuzalisha megawati 50 ikiwa ni utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi.
View
Mradi wa kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere umejengwa katika maporomoko ya mto Rufiji umekamilika na una uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2,115.