11 EAST AFRICAN PETROLEUM CONFERENCE AND EXHIBITION 11
View
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Kushoto) na Waziri wa Miundombinu wa Rwanda Mhe. Dkt. Jimmy Gasore (Kulia) wakisaini makubaliano ya ushirikiano kwenye Sekta ya Nishati kati ya Nchi hizo mbili, katika ukumbi wa Mikutano wa Kigali (KCC) uliopo Kigali, Rwanda.
View
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi katika matukio mbalimbali kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa kilovoti 220 kutoka Benaco hadi Kyaka na ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Benaco Wilaya ya Ngara mkoani Kagera.
View
Mhe. Deogratius Ndejembi (Kulia) Waziri wa Nishati Tanzania akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Dkt. Kgosientsho Ramokgopa Waziri wa Umeme na Nishati Afrika Kusini mara baada ya kushiriki Mkutano wa tano (5) wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika wanashughulikia Nishati na Uchukuzi uliofanyika Jijini Johannesburg, Afrika Kusini, ambapo walikubaliana kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Nishati kati ya Nchi hizo mbili.
View
Mhe Deogratius Ndejembi Waziri wa Nishati Tanzania (kulia) na Mhe. Opiyo Wandayi (Kushoto) Waziri wa Nishati na Petroli wa Jamhuri ya Kenya wakisaini makubaliano ya ushirikiano ya kuanza mauziano ya umeme baina ya Nchi hizo na upembuzi yakinifu wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Dar es Salaam hadi Mombasa. Ikulu Jijini Dar es Salaam.
View
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam mara baada ya kukabidhi mradi wa Nishati safi ya Kupikia shuleni hapo.
View
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akipika kwa kutumia Nishati safi ya Kupikia katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam mara baada ya kukabidhi mradi huo.
View
Minister for Energy Hon. Deogratius Ndejembi, receiving technical briefing from Tanzania Electric Supply Company Limited (TANESCO) Engineer during his inspection visit of Mahumbika Substation in Lindi Region, which has a capacity of 35MVA.
View
Waziri wa Nishati Mhe, Deogratius Ndejembi akiwa katika picha ya pamoja wakati akizindua mradi wa uchimbaji wa visima vitatu ambapo viwili ni kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay na kimoja kwa ajili ya utafutaji huku utekelezaji umefikia asilimia 58 tarehe 27 Februari 2026 mkoani Mtwara
View
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amezindua mradi wa kusambaza mifumo ya umeme jua visiwani unaolenga kuweka mifumo 20,000 ya umeme jua katika visiwa 120 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 8 ambapo Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan ameweka ruzuku hadi ya asilimia 75 katika gharama za uunganishaji umeme.
View
Mradi wa umeme jua wa Kishapu mkoani Shinyanga utakaozalisha megawati 150. Kwa sasa mradi umeanza kuzalisha megawati 50 ikiwa ni utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi.
View
Mradi wa kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere umejengwa katika maporomoko ya mto Rufiji umekamilika na una uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2,115.