MAKAMBA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA WIZARA YA NISHATI KATIKA MJI WA SERIKALI, DODOMA
MAKAMBA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA WIZARA YA NISHATI KATIKA MJI WA SERIKALI, DODOMA
Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba tarehe 01/03/2023, amekagua Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo katika mji wa Serikali Mtumba.
Waziri Makamba aliambatana na Wakurugenzi Wasaidizi Sehemu ya Utawala.
Ujenzi wa jengo la Wizara umefikia asilimia 58.
Kwa sasa Mkandarasi- Shirika la Nyumba la Taifa (NHC ) anamalizia upigaji wa lipu na anaendelea na hatua nyingine za kumalizia ujenzi.