MHA. MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO SABASABA.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), na kampuni zake Tanzu katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mha.Mramba ametembelea banda hilo ili kuona huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.