Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati wa Tanzania, Mhe. Dkt. Doto Biteko (kulia) pamoja na Mhe. Ruth Nankabirwa, Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Jamhuri ya Uganda wakionyesha mikataba mahsusi iliyosainiwa na viongozi hao kwa ajili ya upembuzi yakinifu ujenzi wa Bomba la Gesi kutoka Tanzania kwenda Uganda.Mkataba umesainiwa leo jijini Dodoma.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko (kulia) akizungumza na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dkt. Michael Battle, katika Ofisi ndogo za Wizara ya Nishati Jijini Dar es Salaam, Septemba 13, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Mhe. Judith Salvio Kapinga kuwa Naibu Waziri wa Nishati katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu ndogo Tunguu Zanzibar tarehe 01 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu (Uratibu wa Shughuli za Serikali) na Waziri wa Nishati katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu ndogo Tunguu Zanzibar tarehe 01 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivuta kamba pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Kikagati – Murongo, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023. Mradi huo wa umeme utanufaisha nchi zote mbili katika masuala ya Nishati ya umeme.
MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA KUZALISHA UMEME WA JULIUS NYERERE (JNHPP) UTAKAOZALISHA MEGAWATI 2,115
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) akishuhudia mabadilishano ya mikataba baina ya Mkurugenzi Mkuu wa REA Mhandisi Hassan Saidy (wa pili-kulia) na Mkandarasi kutoka Kampuni ya Dieynem (wa pili-kushoto) baada ya kusaini moja ya mikataba ya kupeleka umeme vijijini. Tukio hilo lilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, Februari 14, 2023. Wa kwanza kulia ni Mwanasheria wa REA, Mussa Muze
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu akishuhudia Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Maharage Chande na Mwanasheria wa Shirika hilo, Zaharani Kisilwa wakibadilishana mikataba ya uimarishaji gridi na wakandarasi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akibonyeza Kitufe kuashiria Hatua ya Kufunga Njia ya Kuchepusha Maji na Kuanza Ujazaji wa Maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme (Megawati 2115) la Julius Nyerere JNHPP kwenye Mto Rufiji Mkoani Pwani tarehe 22 Desemba, 2022.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba (wa sita kulia) pamoja na ujumbe alioambata nao wakiangalia kazi ya usimamishaji wa nguzo za umeme zitazotumika kusafirisha umeme kutoka Mradi wa Rusumo hadi Kituo cha Umeme cha Nyakanazi, wakati wa ziara ya kukagua kituo cha hicho na njia ya kusafirisha umeme kutoka Mradi wa Rusumo, Julai 6, 2022, mkoani Kagera.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba( katikati) na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Emmanuel Tutuba( watatu kushoto) wakioneshwa eneo la mradi wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa kuzalisha umeme wa RUSUMO, Julai 5, 2022 mkoani Kagera
Kituo cha Mafuta cha TANOIL kilichopo Mkoa wa Iringa.
Muonekano wa mtambo wa kuchoronga kisima cha gesi asilia katika kitalu cha SongoSongo ulipofanyika mradi wa ukarabati wa visima.
Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba akigusa maji ya moto yanayotoka katika kisima kifupi cha utafiti cha Jotoardhi kilichochorongwa katika eneo la Kiejo-Mbaka wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Kulia kwake ni Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Mathew Mwangomba.
Frea ikiashiria uwepo wa gesi katika kiwanda cha kuchakata gesi asilia Madimba Mtwara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitia saini mkataba wa Tamko la Pamoja kati ya Tanzania na Uganda kuhusu utekelezaji wa pamoja wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki kutoka Hoima (Uganda) hadi Chongoleani Tanga
Maporomoko ya maji ya Mto Malagarasi yatayozalisha umeme wa megawati 49.5
Mmoja wa wafaidika wa usambazaji Gesi Asilia majumbani, wilayani Kinondoni akitumia gesi hiyo kupikia.
Mradi wa umeme wa upepo wa Mwenga unaozalisha megawati 2.4 wilayani Mufindi mkoani Iringa
Kituo cha kujazia Gesi asilia katika magari (CNG) ya kampuni ya kutengeneza Saruji ya Dangote mkoani Mtwara.
Muendelezo wa tafiti za nishati ya Jotoardhi katika Mradi wa Ngozi, mkoani Mbeya.
Mitambo ya kupokelea Gesi asilia katika eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam.
Shule ya Sekondari Mlewa wilayani Manyoni ambayo imeunganishiwa umeme kupitia Mradi wa REA III mzunguko wa kwanza.
Mitambo ya umeme katika kituo cha umeme cha Dege wilayani Kigamboni mkoani Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa akiangalia sehemu ya ujenzi wa mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), na kuzindua uchepushaji wa maji ya mto Rufiji, kupisha ujenzi wa tuta kuu la bwawa la kufua umeme mkoani Pwani, Novemba 18, 2020.