Mradi wa kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere umejengwa katika maporomoko ya mto Rufiji umekamilika na una uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2,115.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akikagua mitambo mbalimbali ya umeme wa Gesi mara baada ya kutembelea Kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi Julai 10, 2025 jijini Dar es salaam.
Mitambo ya umeme wa Gesi Asilia, katika kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi kilichopo jijini Dar es Salaam.
Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia umeme na nishati Jadidifu, Dkt Khatibu Kazungu wa pili kushoto na Balozi wa Umoja wa Ulaya Mhe. Balozi Christine Grau(katikati) wakizindua hafla ya ugawaji wa magari mawili kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili ya kuanza kampeni ya kutoa elimu ya uhamasishaji wa nishati safi ya kupikia nchi nzima, tarehe 04 Julai, 2025
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko
(katikati) akizindua Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati ya
Kupikia jijini Dodoma tarehe 2 Juni 2025. Kulia kwake ni Naibu Waziri
wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, kushoto ni Lamine Diallo ambaye ni
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu kutoka Umoja wa Ulaya (EU).
Naibu Waziri wa Nishati Mh.Judith Kapinga akizindua kituo Mama cha gesi asilia iliyoshindiwa (CNG) ambacho kina uwezo wa kujaza Gesi Asilia kwenye magari 1200 kwa siku,Mei 9, 2025.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko(wa nne toka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mawaziri wa Nishati wa nchi wanachama wa Umoja wa Soko la pamoja la Kuuziana Umeme katika ukanda wa Mashariki mwa Afrika (EAPP) mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa 20 wa Baraza la Mawaziri wa Nishati wa nchi Wanachama wa Umoja wa Soko la Pamoja la Kuuziana Umeme katika Ukanda wa Mashariki mwa Afrika (EAPP), mkutano huo umefanyika 17 Aprili 2025 Jijini Kampala, Nchini Uganda