Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivuta kamba pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Kikagati – Murongo, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023. Mradi huo wa umeme utanufaisha nchi zote mbili katika masuala ya Nishati ya umeme.
MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA KUZALISHA UMEME WA JULIUS NYERERE (JNHPP) UTAKAOZALISHA MEGAWATI 2,115
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) akishuhudia mabadilishano ya mikataba baina ya Mkurugenzi Mkuu wa REA Mhandisi Hassan Saidy (wa pili-kulia) na Mkandarasi kutoka Kampuni ya Dieynem (wa pili-kushoto) baada ya kusaini moja ya mikataba ya kupeleka umeme vijijini. Tukio hilo lilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, Februari 14, 2023. Wa kwanza kulia ni Mwanasheria wa REA, Mussa Muze
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu akishuhudia Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Maharage Chande na Mwanasheria wa Shirika hilo, Zaharani Kisilwa wakibadilishana mikataba ya uimarishaji gridi na wakandarasi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza, Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba kuhusu Kituo cha Kusafirishia Umeme (Switchyard) katika Mradi wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) katika Mto Rufiji Mkoani Pwani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akibonyeza Kitufe kuashiria Hatua ya Kufunga Njia ya Kuchepusha Maji na Kuanza Ujazaji wa Maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme (Megawati 2115) la Julius Nyerere JNHPP kwenye Mto Rufiji Mkoani Pwani tarehe 22 Desemba, 2022.
Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba akitazama mmoja wa mitambo ya bayogesi iliyopo katika Shule ya Sekondari ya Queens of Family iliyopo Kahama mkoani Shinyanga.Shule inatumia nishati ya bayogesi ajili ya kupikia.
Bi. Marian Sitta, Mwenyekiti wa Mamalishe katika eneo la Kagongwa wilayani Kahama, akiwasha jiko la gesi tayari kwa matumizi baada ya kukabidhiwa jiko hilo na Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba ikiwa ni programu maalumu ya majaribio ambayo itawezesha upatikanaji wa taarifa zitakazozewesha kutengeneza mkakati wa kitaifa wa usambazaji wa gesi nchini.
Waziri wa Nishati, January Makamba akizungumza na Kikundi cha Mamalishe Busisi ikiwa ni sehemu ya umasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo aliwapatia pia mitungi ya gesi kurahisisha shughuli zao na kuepukana na athari za kuni na mkaa, Julai 14,2022.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba (wa sita kulia) pamoja na ujumbe alioambata nao wakiangalia kazi ya usimamishaji wa nguzo za umeme zitazotumika kusafirisha umeme kutoka Mradi wa Rusumo hadi Kituo cha Umeme cha Nyakanazi, wakati wa ziara ya kukagua kituo cha hicho na njia ya kusafirisha umeme kutoka Mradi wa Rusumo, Julai 6, 2022, mkoani Kagera.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba( katikati) na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Emmanuel Tutuba( watatu kushoto) wakioneshwa eneo la mradi wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa kuzalisha umeme wa RUSUMO, Julai 5, 2022 mkoani Kagera
Waziri wa Nishati, January Makamba akimwelekeza Agnes Doto, mkazi wa mtaa wa viwandani wilayani Bariadi jinsi gesi ya mitungi inavyofanya kazi na faida zake baada ya kutumia nishati hiyo safi ikiwemo kujiepusha na magonjwa katika mfumo wa hewa, Julai 13,2022.
Waziri wa Nishati, January Makamba akizungumza na wanachi katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe alipofika kisiwani humo kutatua changamoto ya upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia,Julai 12,2022.
Kituo cha Mafuta cha TANOIL kilichopo Mkoa wa Iringa.
Muonekano wa mtambo wa kuchoronga kisima cha gesi asilia katika kitalu cha SongoSongo ulipofanyika mradi wa ukarabati wa visima.
Naibu Waziri wa Nishati, Stephen Byabato na Okaasai Opolot, Waziri wa Nchi (Nishati ) wa Uganda baada ya kusaini Kikao cha Kwanza cha Mawaziri kuhusu Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Tanzania hadi Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimshuhudia Waziri wa Nishati January Makamba wakati akiweka Saini Mkataba wa Makubaliano kwenye masuala ya Nishati (Oil and Gas) kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Oman kupitia Wizara ya Nishati na Madini (Sekta ya Madini) ya nchi hiyo katika hafla iliyofanyika Al Bustan, Muscat nchini Oman tarehe 13 Juni, 2022
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akishuhudia utiaji saini Mkataba wa Awali wa Mradi wa kuchakata na kusindika Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas – LNG Project) kwenye Hafla iliyofanyika tarehe 11 Juni 2022 Ikulu, Chamwino Dodoma
Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba akigusa maji ya moto yanayotoka katika kisima kifupi cha utafiti cha Jotoardhi kilichochorongwa katika eneo la Kiejo-Mbaka wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Kulia kwake ni Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Mathew Mwangomba.
Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba (kushoto) akionyesha takwimu za matumizi ya umeme nchini katika Kipindi cha Mwaka Mmoja wa Mama kinachorushwa na Azam TV kuhusu mafanikio ya Sekta ya Nishati Katika Mwaka Mmoja wa Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita, Machi 24, 2022 mkoani Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati, January Makamba (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) hapa nchini, Manfredo Fanti, baada ya kufanya mazungumzo Mkoani Dar es Saalam, Novemba 17, 2021.
Waziri wa Nishati, January Makamba (kulia) akizungumza na Kaimu Balozi wa Saud Arabia nchini Tanzania, Fahd Al-harbi wakati wa kikao na balozi huyo mkoani Dar es Saalam, Novemba 16, 2021.
Waziri wa Nishati, January Makamba (kulia) akizungumza na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Anders Sjoberg wakati wa kikao na Balozi huyo mkoani Dar es Saalam, Novemba 16, 2021.
Waziri wa Nishati, January Makamba (kulia) akizungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati mkoani Dar es Saalam, Novemba 16, 2021.
Waziri wa Nishati, January Makamba ( kulia) na Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Richard Kabonero wakizungumza mkoani Dar es Saalam, Novemba 15, 2021.