SIKU YA NISHATI
Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Nishati, Petro Lyatuu (katikati, waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Nishati waliohudhuria Kongamano la Siku ya Nishati lililofanyika jijini Dar es Salaam sambamba na Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SabaSaba). Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), Mhandisi Charles Sangweni na kulia kwake ni Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Nishati Jadidifu, Mhandisi Imani Mruma.