Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi akipata maelezo kuhusu mfumo wa Kidigitali wa Kupanga na kusimamia miradi ya REA (REA Digital Platform) wakati alipotembelea Banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba na Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy