Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mpomvu Mkoani Geita, kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mpomvu kiligharimu takribani Shilingi 50B kina uwezo wa kusambaza takribani megawati 90 za umeme hivyo kuimarisha hali ya umeme kwa wakazi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa katika Mikoa ya Geita, Kagera, Mwanza na Kigoma, Ujenzi wa kituo hicho ulianza 2019 na kukamilika 2020 na kilizinduliwa rasmi 2022 na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.